Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa;
Kukubali neno lake
Nina raha moyoni.
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa,
Kuamini damu yake
Nimeoshwa kamili.
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa,
Kwake daima napata
Uzima na amani.
Nafurahi kwa sababu
Nimekutegemea;
Yesu,Mpendwa na Rafiki
Uwe nami dawamu.
No comments:
Post a Comment