Thursday, December 8, 2016

58.Mwamba Wenye Imara


Mwamba wenye imara
Kwako nitajificha!
Maji hayo na damu
Yaliyotoka humu,
Hunisafi na dhambi,
Hunifanya mshindi.

Kwa kazi zote pia ,
Sitimizi sharia.
Nijapofanya bidii,
Nikilia nakudhii,
Hayaishi makosa;
Ndiwe wa kuokoa.

Sina cha mkononi,
Naja Msalabani;
Nili tupu, nivike;
Ni mnyonge, nishike;
Nili mchafu naja,
Nioshe nisijafa.

Nikungojapo chini,
Nakwenda kaburini;
Nipaapo Mbinguni,
Na kukwona enzini:
Roho yangu na iwe
Rahani mwako wewe.

No comments:

Post a Comment