Thursday, December 8, 2016

55.Nipe Moyo Wenye Sifa


Nipe moyo wenye sifa
Sio wa utumwa;
Moyo ulionyunyizwa
Damu ya thamani.

Moyo msikizi, moyo
Wa kunyenyekea,
Moyo utawaliwao
Na Mwokozi pia.

Mwenye kutubu, mnyonge,
Sadiki, amini;
Kamwe, kamwe asitengwe
Akaaye ndani.

Mpya, mwema na mawazo
Mwingi wa mapenzi
Nawe uwe kielelezo
Moyo wa Mwokozi.

Ni uule moyo wako;
Moyo wa huruma
Yesu, natamani kwako
Kukujua vyema.

Na ya midomo matunda
Yako, nipe nami;
Amani isiyokoma
Iwe yangu mimi.

Nitie yako tabia,
Inishukie juu;
Jina lako nipe pia,
Ndilo la upendo.

Ni wa baba utukufu;
Mwana atukuke;
Na roho Mtakatifu
U utatu pweke.

No comments:

Post a Comment