Nipe moyo wenye sifa
Sio wa utumwa;
Moyo ulionyunyizwa
Damu ya thamani.
Moyo msikizi, moyo
Wa kunyenyekea,
Moyo utawaliwao
Na Mwokozi pia.
Mwenye kutubu, mnyonge,
Sadiki, amini;
Kamwe, kamwe asitengwe
Akaaye ndani.
Mpya, mwema na mawazo
Mwingi wa mapenzi
Nawe uwe kielelezo
Moyo wa Mwokozi.
Ni uule moyo wako;
Moyo wa huruma
Yesu, natamani kwako
Kukujua vyema.
Na ya midomo matunda
Yako, nipe nami;
Amani isiyokoma
Iwe yangu mimi.
Nitie yako tabia,
Inishukie juu;
Jina lako nipe pia,
Ndilo la upendo.
Ni wa baba utukufu;
Mwana atukuke;
Na roho Mtakatifu
U utatu pweke.
No comments:
Post a Comment