Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.
Yesu, nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe, Mwokozi,
Nakujia.
Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.
Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.
Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.
Nina haja nawe,
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.
No comments:
Post a Comment