Thursday, December 8, 2016

11.Nina haja nawe


Nina haja nawe
Kila saa;
Hawezi mwingine
Kunifaa.

Yesu, nakuhitaji
Vivyo kila saa!
Niwezeshe, Mwokozi,
Nakujia.

Nina haja nawe;
Kaa nami,
Na maonjo haya,
Hayaumi.

Nina haja nawe;
Kila hali,
Maisha ni bure,
Uli mbali.

Nina haja nawe,
Nifundishe
Na ahadi zako
Zifikishe.

Nina haja nawe,
Mweza yote,
Ni wako kabisa
Siku zote.

No comments:

Post a Comment