Thursday, December 8, 2016

1.Mwokozi Umeokoa

Mwokozi umeokoa,
Nimekuwa wako wewe.
Damu imenisafisha;
Sifa kwa mwana Kondoo.

Utukufu, Aleluya!
Sifa kwa Mwana Kondoo!
Damu imenisafisha,
Utukufu kwa Yesu!

Nilijitahidi sana
Ila sikupata raha;
Bali kwa kumtegemea
Nilipata Baraka.

Daima namwegemea
Damu ikifanya kazi,
Nikioga kwa chemichemi
Itokayo Mwokozi.

Sasa nimewekwa wakfu;
Nitaishi kwako wewe:
Fahari nashuhudia
Ya wokovu wa bure.

Nasimama kwake Yesu,
Ameponya roho yangu;
Ameniondoa dhambi,
Anifanye mzima.

Nilikuwa kifungoni,
Niliteswa na dhambi,
Nilifungwa minyororo
Yesu akanifungua.

Sifa, ameninunua!
Sifa, nguvu za wokovu!
Sifa, Bwana huhifadhi!
Sifa zake milele.

No comments:

Post a Comment