Thursday, December 8, 2016

7.Ni Tabibu Wa Karibu


Ni tabibu wa karibu;
Tabibu wa ajabu;
Na rehema za daima;
Ni dawa yake njema.

Imbeni, malaika,
Sifa za Yesu Bwana;
Pweke limetukuka
Jina lake Yesu.

Hatufai kuwa hai,
Wala hatutumai,
Ila kweli yeye ndiye
Atupumzishaye.

Dhambi pia na hatia
Ametuchukulia;
Twendeni na amani
Hata kwake Mbinguni.

Huliona tamu jina
La Yesu Kristo Bwana,
Yuna sifa mwenye kufa
Asishindwe na kufa.

Kila mume asimame,
Sifa zake zivume;
Wanawake na washike
Kusifu jina lake.

Na vijana wote tena,
Wapendao sana
Waje kwake wawe wake
Kwa utumishi wake.


No comments:

Post a Comment