Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Kila tukiamka tunakuabudu
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi,
Ewe Utatu, tunakusifu.
Baba, Mwana, Roho, wakuaminio
Wanakutolea shukrani zao
Wanakusujudia malaika nao:
Wewe u mwanzo, nawe u mwisho.
Baba, Mwana, Roho, sisi tu gizani,
Utukufu wako hatuoni kosa;
U Mtakatifu, nawe u mapenzi,
U peke yako, mwenzio huna.
Baba, Mwana, Roho, Mungu mwenye enzi,
Ulivyoviumba vyote vyakusifu:
Baba, Mwana, Roho, Mungu wa mapenzi
Ewe Utatu, tunakusifu.
No comments:
Post a Comment