Thursday, December 8, 2016

30.Nilikuwa kondoo aliyepotea


Nilikuwa kondoo aliyepotea,
Sikupenda zizi kamwe, ila kutembea
Nilikuwa mwana asiyesikia,
Sikupenda baba yangu wala kutulia.

Na mchunga mwema alinitafuta,
Baba kwa mapenzi ndiye aliyenivuta;
Karibu ya kufa, kwa kiu na kwa njaa,
Waliniona mnyonge, waliniokoa.

Yesu ni mchunga, mwenziwe hapana,
Aliosha taka zangu, dhambi nyingi sana;
Kwa vidonda vyangu alitia dawa.
Ndiye aliyenipata, na kwake nalindwa.

Nilikuwa kondoo aliyepotea
Sasa nampenda Baba, na mchunga pia;
Kwanza nilitanga na kukosa sana,
Hivi nyumbani mwa Baba sipotei tena.

No comments:

Post a Comment