Peleleza ndani yangu,
Iwe safi nia,
Kwangu kama kwako Mungu,
Idhihiri pia.
Peleleza moyo wangu
Uunifunulie,
Yaliyomo ndani yangu
Nami niyajue.
Kwanza washe zako tambi,
Kumefunga giza;
Nijue ambavyo dhambi
Ni la kuchukiza.
Peleleza na mawazo
Ni mbegu za mambo,
Asili ya machukizo,
Maumbuo – umbo.
Zidi kuyapeleleza
Katikati yangu
Hata wishe nifundisha
Udhaifu wangu.
Hapo nikikwinamia
Mbele zako, Mungu,
Hakika nitakujua
U mpenzi wangu.
No comments:
Post a Comment