Thursday, December 8, 2016

26.Yesu Unipendae


Yesu unipendaye
Kwako nakimbilia,
Ni wewe utoshaye,
Mwovu akinijia;
Yafiche ubavuni,
Mwako maisha yangu;
Nifiikishe mbinguni
Wokoe moyo wangu.

Ngome nyingine sina;
Nategemea kwako.
Usinitupe Bwana ,
Nipe neema yako,
Ninakuamania
Mwenye kuniwezesha;
Shari wanikingia,
Vitani wanitosha.

Nakutaka Mpaji
Vyote napata kwako;
Niwapo muhitaji,
Utanijazi vyako;
Nao waangukao
Wanyonge wape nguvu;
Poza wauguao,

Uongoze vipofu.
Bwana umeniosha
Moyo kwa damu yako;
Neema ya kutosha
Yapatikana kwako;
Kwako Bwana naona
Kisima cha uzima;
Mwangu moyoni Bwana,
Bubujika daima.

No comments:

Post a Comment