Thursday, December 8, 2016

33.Dhambi Ikikulemea


Dhambi ikikulemea,
Kwa Bwana rehema;
Hivi sasa tegemea
Neno la salama.

Tegemea, tegemea,
akwita sasa.
Ni Mwokozi, ni
Mwokozi; amini sasa.

Yesu amemwaga damu
Ya nyingi baraka;
Nawe sasa oga mumu
Zioshwamo taka.

Ni njia yeye hakika
Hwongoza rahani;
Usikawe kumshika,
Uwe barakani.

Karibu nawe wingie
Mwetu safarini,
Twende tukamwamkie,
Milele Mbinguni.

No comments:

Post a Comment