Kwa wingi wa nyama,
Na sadaka pia,
Hupata wapi salama,
Kwondoa hatia?
Sadaka ni Yesu,
Hwondoa makosa;
Dhabihu mwenye jina kuu,
Atanitakasa.
Kwa yangu imani,
Nikuweke sasa
Mkono mwako kichwani
Kukiri makosa.
Roho yakumbuka
Mambo ya mtini,
Mzigo ulijitweka,
Ndiyo yangu deni.
Deni hutanguka,
Tukimuamini;
Kwa damu tumeokoka,
Twimbe furahani.
No comments:
Post a Comment