Thursday, December 8, 2016

65.Safari


Katika safari yetu
Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini.

Ng’oani! Tujifungeni,
Twende zetu juu!
Kristo ndiye kiongozi;
Tusihofu tu.

Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.

Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.

Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.

Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika.

No comments:

Post a Comment