Katika safari yetu
Kwenda Mbinguni
Tusiishe siku zetu
Usingizini.
Ng’oani! Tujifungeni,
Twende zetu juu!
Kristo ndiye kiongozi;
Tusihofu tu.
Atwekwe badala yetu,
Mwenyewe Bwana;
Yesu kiongozi wetu
Atapokea.
Kisimani, maji tele,
Maji mazima!
Maji hayo,
Ya milele
Yana neema.
Njiani miiba mingi,
Yatuumiza;
Hofu na hatari nyingi,
Sana zakaza.
Kweli, njia ya Mbinguni
Ni ya mashaka;
Tuwe na Yesu njiani,
Mara hufika.
No comments:
Post a Comment