Tuesday, December 6, 2016

117.Tufani Inapovuma


Tufani inapovuma
Sana moyoni mwangu,
Huona pa kujificha
Mkononi mwa Mungu.

Hunificha, hunificha
Adui hatanipata,
Hunificha, hunificha,
Mkononi mwake.

Pengine kuna taabu
Yanisongeza kwake;
Naijua si hasira,
Ni ya mapenzi yake.

Adui wakiniudhi
Nami nikisumbuka,
Mungu atavigeuza
Vyote viwe baraka.

Niishipo duniani
Ni tufani daima,
Anilindapo rohoni
Nitakaa salama.

No comments:

Post a Comment