Tufani inapovuma
Sana moyoni mwangu,
Huona pa kujificha
Mkononi mwa Mungu.
Hunificha, hunificha
Adui hatanipata,
Hunificha, hunificha,
Mkononi mwake.
Pengine kuna taabu
Yanisongeza kwake;
Naijua si hasira,
Ni ya mapenzi yake.
Adui wakiniudhi
Nami nikisumbuka,
Mungu atavigeuza
Vyote viwe baraka.
Niishipo duniani
Ni tufani daima,
Anilindapo rohoni
Nitakaa salama.
No comments:
Post a Comment