Sunday, December 4, 2016

127.Bwana Yesu Atakuja

Bwana Yesu atakuja, Vumilia!

Omba, ukiwa na haja, Vumilia!

Mbingunu Mungu aliko, Mwamini Mwokozi wako,

Nawe utafika huko, Vumilia!

Ikikucheka dunia, Vumilia!

Mwovu atakuvizia, Vumilia!

Hataweza kukushinda, Bwana Yesu akulinda,

Roho yako, akupenda, Vumilia!

Na ukiwa hatarini, Vumilia!

Dhiki nyingi duniani, Vumilia!

Vyatupasa kuyakuta, Majaribu na matata,

Na Bwana hakutuficha; Vumilia!

Adui wakikutana, Vumilia!

Na ndugu wakikukana, Vumilia!

Zote, zote zitakwisha, Nguvu zote za kutisha

Mungu chini atashusha; Vumilia!

Moyoni una majonzi, Vumilia!

Ndiyo bonde-ya-machozi, Vumilia!

Hima tutaandamana, Kwetu Mbinguni na Bwana

Tena hatutaachana; Vumilia!

No comments:

Post a Comment