Neno lako, Bwana,
Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.
Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.
Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.
Ukiliamini,
Hwenda na amani;
Una na furaha
Neno ni siraha.
Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana
Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja I papo,
Tufarikanapo.
No comments:
Post a Comment