Tuesday, December 6, 2016

111.Neno,Lako Bwana


Neno lako, Bwana,
Ni imara sana;
Lilo latwongoza,
Lilo latufunza.

Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.

Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.

Ukiliamini,
Hwenda na amani;
Una na furaha
Neno ni siraha.

Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana

Neno la rehema,
Tukali wazima;
Faraja I papo,
Tufarikanapo.

No comments:

Post a Comment